Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekabidhi leseni za kufanya huduma ya kutoa habari kwa njia ya mtandao kwa Blogs, Online TV na Online Redio ambazo zimekamilisha usajili. Bongo5 na Michuzi pamoja na Lemutuz ni moja kati ya Blogs na Online TV ambazo zimekabidhiwa leseni ya kufanya huduma hizo huku baadhi ya blogs kama Muungwana, Millardayo, Mwanaharakati na nyingine nyingi zikipewa leseni ya kurusha matangazo kupitia blogs pekee.