Taarifa kutoka katika tovuti ya Ubalozi wa Marekani leo November 13, 2018 imeandikwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo inasema "Serikali ya Marekani imesikitishwa sana na matukio ya mashambulizi yanayoshamiri na hatua za kisheria zinazochukuliwa na serikali ya Tanzania, ambazo zinakiuka uhuru wa raia na haki za binadamu, na zinazojenga mazingira ya vurugu, vitisho na ubaguzi."